Friday, May 31, 2013

Haya sasa...

Habari! Naomba unipostie ujumbe wangu kwenye blog yako,




Mimi ni mkaka wakitanzania naishi dar, natafuta mwanamke mtu mzima mwenyehitaji lakupendwa tupendane na kiu zetu za mapenzi tutimiziane kwa raha na uhuru wetu,



Nina miaka 38, yeye awe umri kuanzia miaka 40 kundelea, ambae yuko tayari awasiliane nami kwa e mail erickytz@yahoo.com



Home's Boss Lady



UTASA....

Leo nataka kuongelea hili swala la utasa, jamani tunajuwa wote hata kama mnapendana kiasi gani na mkaoana ikifika wakati mmeshindwa kupata mtoto hapo ndipo ugomvi mkubwa na hata kuachana kunapojitokeza, ila kwa wapendanao wachache sana wanaopendana kwa kweli na kwa moyo mmoja huwa wanavumiliana na kutafuta njia mbadala tena wakifichiana aibu.

Nakumbuka nina baba yangu mdogo mmoja yeye na mkewe walioana na kukaa miaka 14 bila mtoto maneno yalikuwa mwengi sana kwenye familia lakini yule baba katu hakusikiliza maneno ya mtu aliendelea kuwa na kumtumikia mkewe kwa moyo mmoja wakiomba MUNGU siku awape mtoto ndipo mwaka wa 14 ya ndoa yao wakapata mtoto mmoja.

Naingia kwenye biblia sasa tunaona ya kwamba mke wa Ibrahimu hakubahatika kupata mtoto kwa muda mrefu mpaka alipokuwa na miaka 80 na hivyohivyo Isaka mtoto wa Ibrahimu alipomuoa Rebeka walikaa muda mrefu bila kupata mtoto lakini hawakukata tamaa walimuomba MUNGU naye akawapa mtoto.

Utasa unaweza ukawa umerithiwa katika ukoo kuna koo nyengine hawana vizazi vingi utakuta wamezaa watoto wachache sana na wengine hawana watoto kabisa, wewe baba ukikuta mkeo hana ama hapati mtoto kwa muda mrefu kuliko uanze kumuandama na ndugu zako ama kwenda kuzaa nje hebu tafakari ule upendo mliokuwa nao mwanzo, na tafakari MUNGU alivyokubariki ukapata mke au unadhani maujuzi yako tu ndio yamekupa mke kwani kabla hujaoa siulikuwa na wanawake wengine mbona hukuoa hao bali huyo uliyenaye ndio chaguo lako MUNGU alilokupa.

Basi tumuheshimu na kuzidi kumuomba atakupa baraka za watoto, wakati wa kipindi kigumu mnachopitia kwenye familia upendo wa ukweli mliokuwa nao kwenu ndio utawasaidia kuvuka majaribu, ila unapogeuka na kumchukulia mwenzako poa poa inaweza kuharibu kila mpango katika maisha yako na hata usielewe na kuona umhumu wa kwanini ulioa.

Tafakari

Sifa ya mwanamke nyonga...Kajitegemee

Unaambiwa mchina kaleta vitu vingi feki nywele, makalio, hips, kope, yani vitu kibao ila kashindwa kutengeneza nyonga feki..haloooooooooooooo mwanamke kunyongesha ndio starehe ya mzunguko na heshima ya mwili wako..akijetegemeee na kama huwezi nitafute tukufundishe..

Walio kuja kufundwa mwezi wa nne walifundishwa kukata nyonga natumaini bado wanaendeleza makamuzi..haya na nyie wamama mliolewa wenye nyumba zenu aka wamama wenye nyumba kazi kwenu sasa 7/7/2013 tukanyongesheeee...hahahaha hatareeeeeeeeeeeeeeee

Wednesday, May 29, 2013

Home's Boss Lady...

Kuelekea siku yetu ya kufunda wanawake walioolewa na kutambua umuhimu wa wewe kuwa mke mpaka siku yetu ikifika kila mara nitakuwa natuma humu picha za wanawake walioolewa katika siku yao ya harusi na kama wewe pia unapenda kunitumia picha yako ya harusi unakaribishwa tuma picha zako kwenda rosemarymizizi@yahoo.com

Naamini jinsi utakavyokuja siku hiyo sio jinsi utakavyondoka siku hiyo najuwa utaondoka na nguvu na upendo mpya wa kwenda kuwa mama na mke bora katika familia yako, karibuni sana


Tuesday, May 28, 2013

Mapito ya ndoa na Mashoga....

Leo nataka niongelee kitu kimoja ambacho nimeona ndoa nyingi sana zikiingia matatizoni na wengine kuachana kwa sababu ya huu uzembe na ndio maana napenda sana kuukazia.

Jamani mashoga ni wazuri sana na nikiongelea mashoga ni marafiki wa karibu wa kike, wengi tunao na wengi pia bila hao mashoga wasingefika mahali walipo, kuna mazuri mengi ambayo mashoga wanaweza kukufanyia na mabaya mengi ambayo pia wanaweza kukufanyia, na hapa nataka na wanaume pia wajifunze kwa marafiki zao wakaribu.

Kabla hujaolewa unakuwa nao wengi sana lakini umeshagundua kwanini wanawake wengi wakishaolewa huwa hawana kabisa mashoga??? sio tu kwasababu wapo busy na familia zao bali hawaoni tena maana yakuendeleza ama kuuweka ushoga mbele kuliko familia zao.

Nasio vizuri kwa mwanamke uliyeolewa ukapata matatizo na mapito katika ndoa yako na ukayapeleka kwa wazazi wako au hata ndugu zako kwani unajenga uwadui wao kumchukia mumeo kwani nani ambaye anapenda mtoto wake apate tabu lazima watakasirika na kumuona mume hana maana, ndio maana napenda kushauri wanawake kwenye ndoa kuwa na mashoga ambao na wao wanandoa ili waweze kutoana mawazo na kupeana nguvu ya kuendelea na ndoa, maana ndoa jamani sio mchezo wa kuigiza kwamba ukicheza hivi leo kesho mnaweza kufuta hicho kipande kwenye script na muweke kingine..ohoooo

Narudia tena muelewe sikatazi mwanamke aliyeolewa kuwa na mashoga ambao hawajaolewa maana kuna vitu kama upatu mnaweza kucheza pamoja kwa ajili ya maendeleo kuna wakati mwengine mnataka tu kutoka muende sehemu muongee na kufurahi, ila kwanini napenda kushauri wanawake walioolewa kuwa na mashoga wengi ambao na wao wameolewa na kutokubali kuwa na mashoga wengi ambao hawajaolewa ni kwasababu zifwatazo.

Kwanza kabisa wote tulio kwenye ndoa tunajuwa mapito ya ndoa yalivyo mengi na kila mtu anapitia hakuna mtu yoyote ambaye yeye ndoa yake ni tambarale tu siku zote ila tu mapito yetu yametofautiana, sasa bas labda wewe mama kwenye ndoa yako mumeo ni mlevi hatari anarudi usiku wa manane amelewa, hela ya matumizi nyumbani haachi anakuambia hana akirudi yupo tilalila umeshamsema na kumshauri lakini habadiliki utafanyaje hapo ndio unamuhitaji rafiki yako fulani mwenye ndoa akufahamishe cha kufanya maana kama yeye halalipitia hilo basi kapitia kitu karibu na hicho na yeye si ana ndoa, sasa wewe kampelekee yule shoga yako anayekula na kulala kwa mama uone atakalokujibu cha kufanya ni wachache sana wenye busara, juzi nimesikia msemo ukimwaga ugali nitamwaga mboga..utafakari kiutu uzima.

huo ni mfano tu ambao utakusaidia kuelewa kwanini huwa napenda kushauri wanawake walioolewa kuwa na mashoga zaidi ambao na wao wameolewa.

NOTE: kwa upande wangu mimi siwezi kumuomba ushauri wa ndoa shoga yangu aliyeachika kwenye ndoa kwakweli siwezi maana kama yeye kashindwa kumudu maumivu ya ndoa atanishauri nini mimi, labda kama ameachika kwenye ndoa kwasababu za kueleweka labda mumewe malaya sana harekebishiki na kashindwa kuvumilia, au mwanaume hana muda na familia yake akaona bora alee watoto wake mwenyewe na sababu nyengine ambazo zinaeleweka, lakini sio mwanaume kachelewa kurudi mara mbili ukalianzisha timbwili na kuondoka..akuuuuu sitaki mawazo yako mimi.

Kama limekuchoma shoga utanisamehe ila ukweli wangu ndio huo...


MAJANGA.....UUwwwiii Sipati Picha

OPARESHENI Fichua Maovu 'OFM' inayoendeshwa na Magazeti ya Global Publishers inaendelea, hivi karibuni mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Ezekiel Malika 'Baba Kulwa' amenaswa gesti na mkewe akiserebuka na shoga aitwaye Aunt Steve na kuibua mtiti mzito, Ijumaa Wikienda limekukusanyia.


Tukio hilo lililovuta umati lilijiri Mei 20, mwaka huu kwenye gesti moja (jina tunalo) iliyopo Mwananyamala, Dar ambapo mke wa Ezekiel alivamia na kutembeza mkong’oto wa hasira kwa mumewe.

ILIKUWAJE?

Mei 19, mwaka huu, saa 3:15 asubuhi, mwanamke mmoja ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa ajili ya heshima yake mtaani alilipigia simu gazeti hili na kutoa malalamiko kwamba mumewe amekuwa na tabia ya kulala na wanaume wenzake ambao ni mashoga.

“Jamani, mimi naitwa… (akataja jina), naomba jina langu lisiandikwe gezetini. Malalamiko yangu ni kwamba, mume wangu amekuwa na tabia ya kulala na mashoga, hivi ninavyoongea ana ahadi ya kukutana na mmoja wao gesti kama si kesho basi keshokutwa, niliona meseji kwenye simu ya mume wangu.

“Nawaomba chondechonde, mnisaidie ili hii tabia ikome. Nipo tayari kusikia maelekezo yenu kwa sababu nimesoma kwenye gazeti lenu kwamba mnafichua maovu na huu nao ni uovu,” alisema kwa masikitiko mwanamke huyo.
MKE APEWA MAELEKEZO

Mratibu wa Oparesheni Fichua Maovu alimpa maelekezo mwanamke huyo akimtaka kufuatilia kwenye simu ya mumewe ili kubaini siku ya wawili hao kukutana gesti.

“Nawaahidi kwamba leo hiihii kabla giza halijaingia nitakuwa nimejua siku yao ya kukutana, naomba msiache kupokea simu yangu jamani.”

OFM: Sawa mama, pole sana.

Mwanamke: Asante sana.

SIMU YASUBIRIWA

Saa 11:00 jioni, mwanamke huyo alipiga simu tena kwa OFM na kupokelewa na yuleyule mratibu wake aliyempa maelekezo.

Mwanamke: Mchana wakati mume wangu amekwenda kuoga niliipekua simu yake, wanakutana kesho kwenye gesti ya …(anaitaja jina).

“Kwa hiyo mtanisaidiaje?”

OFM: Wewe kuwa beneti na mumeo, kesho akiondoka na wewe ondoka hata kwa kujificha, mfuatilie hadi kwenye hiyo gesti huku ukitupa mawasiliano.

Mwanamke: Hilo halina shida, nitakodi Bajaj halafu nitawaambia.

OFM: Oke, kuwa makini, mawasiliano ni muhimu. Tutawanasa kisha wakaishie polisi.

Mwanamke: Nitashukuru sana jamani. Loo! Kweli dunia imekwisha, mwanaume ana mke, hatosheki anatafuta wanaume wenzake, afadhali angekwenda kwa machangudoa.”
 
MKE ACHUKUA MASHOSTI, WATINGA GESTI

Siku ya tukio saa 8:00 mchana, mwanamke huyo akiwa ameongozana na mashoga zake, walifika kwenye gesti hiyo na kubana sehemu ambayo wangeweza kumwona anayeingia na kutoka kisha akawasiliana na mratibu wa OFM ambaye aliwatuma mapaparazi watatu wenye kamera za kupiga picha kwa umbali wa mita 100.

Kufumba na kufumbua, Aunt Steve aliwasili na kuzama ndani ya gesti hiyo kwa kutumia mlango wa nyuma ili asionekane kwa vile sheria ya serikali kuhusu gesti, wanaume hawaruhusiwi kuingia kwenye chumba kimoja.

Mapaparazi wetu wakiwa tayaritayari walitega katika pembe tatu za gesti hiyo ili kunasa tukio hilo hatua kwa hatua.



BABA KULWA NAYE HUYO

Kufumba na kufumbua, Baba Kulwa alitokea na kuingia ndani ya gesti hiyo kwa kutumia mlango mkubwa wa mbele huku akiwa hajui kama arobaini yake ilikuwa imebakiza dakika chache siku hiyo.

Alifika mapokezi na kupewa chumba No. 01, akaenda uani na kufanya jitihada kubwa za kumpitisha shoga huyo kwa mlango wa nyuma hadi ndani.
 
WAACHWA KWA DAKIKA KUMI ILI…

Baada ya wote kuzama chumbani, mke wa mwanaume huyo, mashosti zake na mapaparazi waliwaacha kwa dakika kumi ili wafikie hatua ya kuchojoa nguo hivyo kuweza kuwanasa wakiwa watupu.



MUDA WA MCHEZO WAFIKA

Baada ya dakika kumi, wafumaniaji wote walizama ndani na kugonga mlango wa chumba walichomo wawili hao huku shosti

mmoja wa mwanamke huyo akijitambulisha yeye ni mhudumu anawaongeza taulo. Baba Kulwa bila kufahamu janja hiyo alifungua mlango kidogo na kuchomoza kichwa lakini ghafl a akinadada hao akiwemo mkewe walimvamia na kusukuma mlango, wakazama ndani.



MBILINGE YA NGUVU

Wawili hao walikutwa hawana nguo, ndipo msala ulipomwangukia Baba Kulwa na Aunt Steve wake, mke akipewa nguvu na wapambe wake waliwatembezea kipigo huku wakiwakejeli kwa tukio hilo la aibu.



SHOGA ACHOROPOKA KAMA KAMBALE

Baada ya kuwaweka wote chini ya ulinzi, waliwatoa nje huku Baba Kulwa akiomba msamaha kwa mkewe lakini bila kukubaliwa.

“Msamaha wa nini? We si kidume cha kweli, twendeni nje tukawaanike mbele ya watu,” alisema mwanamke huyo.

Katika hali iliyoonekana ni kukosa umakini wa kuweka kizuizi vizuri, Aunt Steve alifanikiwa kuchoropoka kama samaki aina

ya kambale na kutokomea kusikojulikana huku wanawake hao wakimsindikiza na zomeazomea hadi wakafunga mtaa.
 
NYUMBANI KWA BABA KULWA

Taarifa za katikati ya wiki iliyopita kutoka nyumbani kwa Baba Kulwa zilidai kuwa baada ya kufi ka nyumbani, mwanamke huyo

alikusanya kila kilicho chake na kutimka zake huku mumewe akimbembeleza bila mafanikio.   Source: Global Publishers

Monday, May 27, 2013

I love me some Sheria Ngowi........designs

Leo nilikuwa napitia blog ya 8020 kama kawaida yangu i love this blog na mwenye nayo amenisaidia mengi sana na ananifunza mengi pia..so nikaona hii picha nikagundua kumbe wanaume wengi hupendeza sana wakivaa suits it doesnt matter utaivaa ipi na rangi gani ila hichi kitu bwana hakimkatai mtu..wamevaa vijana wamependeza

Kwa wanaume ambao mnapenda kujichukulia poapoa i have an advice for you wanawake wengi wanapenda wanaume wanaojuwa kuvaa na kujitunza aihusu ukatembea barabarani na mkeo/girlfriend wako ukaanza kusalimiwa kwa heshima ukidhaniwa baba yake mdogo kwa jinsi ulivyoozeeka na mavazi yako..

Wanawake wengi ukimtongoza cha kwanza anaangalia muonekano wako wa nje halafu mengine hufwata baadaye baada ya kukubaliwa, kama mimi nakumbuka enzi za ujana (kabla sijaolewa) mwanaume alikuwa akinitongoza cha kwanza kumwangalia ilikuwa ni viatu, then nguo maana kama huwezi kutunza viatu vyako vinavyokustiri miguu uweze kujitunza utaweza kunitunza miye...nikikuta kimejikunja na kuzeeka jibu ni hapana kabla hata hujaanza sentensi ya pili..

Kwahiyo kwenu wanaume looking sharp ndio habari ya mjini, japo kuwa siku hizi wanawake wengi tunapenda hela kuliko kitu chochote, ngoja niwachekeshe kuna kipindi cha nyuma nilikuwa na marafiki zangu wa kike watatu tukawa sehemu tunazogoa mwenzetu mmoja akasema kwamba ametongozwa na mwanaume sio mzuri ni wa kawaida sana yani hawezi hata kukubali kuolewa naye akimuomba ila tu kwa sababu ana hela zake za haja ndio maana anakuwa naye kwakuwa anamuhonga hatari, sasa mimi kama mnavyonijuwa kwa mdomo nikamuuliza sasa kama anasura mbaya mkiwa kwenye mzunguko inakuwaje humuangalii usoni hahahaha akaniambia wakiwa wapo mafichoni mwao huwa anapokuwa kwenye mzunguko anapenda awekwe style upande atakayoona suruali kwani anajuwa mule kuna hela za kupewa akimalizana na bwana kwahiyo yeye akiwa anazunguka anaiangalia tu ile suruali upande wa wallet..hahahahaha mji huu unahatariiii.

 Nikamwambia sasa inamaana gani kujipa adhabu unazungushwa na mtu humpendi basi bora uwe humpendi kwa muda huo lakini moyoni unajipa moyo utampenda baadaye unatumia nguvu zako huku haufurahii kwasababu ya pesa akaniambia bibi wee kwani sura yake natembea nayo mfukoni sinamuachia mwenyewe cha muhimu ananihudumia basi...hatareeeeee

Hicho ni kibonzo cha leo kwenu nyie wanaume mvuto ni  muhimu kwa maisha haya ya sasa... 


Roho Imeniuma...Mmhhh

Kuna dada mmoja alikuwa ameolewa na wakazaa watoto wawili kwa umri huyu mkubwa anamiaka mitano na mwengine mitatu, kama tunavyojuwa hizi ndoa zinamapito yake na hao kwenye ndoa yao pia walikuwa na mapito ila kwasababu moja ama nyengine hawakuweza kuvumiliana wakaamua kwamba watengane, basi kila mtu akachukuwa hamsini zake.

Yule mama yeye ni mfanya biashara tu ila yule baba anafanya kazi katika bank moja hivi hapa mjini, tokea wameachana yule baba hajawahi kuwaona wala kuwahudumia watoto wake, lakini uzuzri ni kwamba mkewe alikuwa mfanyabiashara japo hakupata faida kubwa ila hakushindwa kuwatunza watoto wake.

Kuna wakati yule mama biashara zake zikawa zinamatatizo hakuwa na hela tena za kujimudu mpaka akafukuzwa kwenye nyumba ambayao alikuwa anakaa na kumuomba rafiki yake akae naye kwa muda ili ajipange, rafiki yake tunakaa naye mabibo ambaye pia nirafiki yangu basi yule mama akaja na watoto wake wakaishi tu vizuri na rafiki yake ambaye huyu rafiki yake yeye ameolewa na ana watoto wawili pia.

Wameishi kwakweli kwa amani na upendo mda wote, lakini huyu mama bado alikuwa na mawazo sana na mumewe kwakuwa alikuwa anampenda bado basi siku zikazidi kwenda lakini baadaye yule mama akaumwa ghafla ugonjwa ukamsababishia sehemu zake nyengine za mwili kufa yaani kuanzia kwenye kiuno kwenda chini pakafa.

Kwakweli nimesikitika sana basi rafiki yake naye alimsaidia sana kumuuguza huyo dada ikaendelea ya kwamba yule mama alizidi kuumwa ikabidi asafirishwe kwa kaka yake ambaye ameoa ili wamuuguze wakamuuguza kwa muda kama miezi miwili lakini yule mke wa kaka yake akaanza kuleta jeuri kwamba hamtaki wifi yake pale ni bora apelekwe kijijini kwa mama yao akauguzwe huko yeye amechoka kumuuguza, kaka yake hakuweza kabisa kumfukuza mdogo wake basi mkewe akamshauri kwakuwa pale kodi inaisha ndani ya miezi miwili basi tutafute nyumba nyengine tumuache hapo huyo dada mpaka kodi ikiisha..ukitaka kujuwa wanawake ni nyoka kweli mumewe akamsikiliza wakaondoka wakamuacha yule dada pale bila msaada wowote.

Mpaka kodi inaisha yule mama alikuwa anaunga unga maisha siku nyengine kaka yake aje amletee msaada siku nyengine hampi anajikokota hivyohivyo afanye kazi zake na MUNGU alikuwa anamsaidia anaweza kupika chakula wakala, akaweza kuwaogesha watoto aliamua kujifunza kwakuwa alijuwa itamchukuwa muda sana kupona ilibidi ajikubali ili aweze kutunza watoto wake.

Mwenye nyumba akaja kudai nyumba yake yule kaka yake akaamua kumchukuwa mdogo wake na watoto wake na kuwapeleka kijijini kwao akauguzwe na mama yao ambaye ni mzee hata yeye anahitaji msaada wa kuangaliwa, lakini kama tunavyojuwa mama ni mama alihangaika kumuuguza mwanye pamoja na watoto wa mwanaye huku yule mama akijitahidi hivyohivyo kuishi maisha yake akiwa nusu hai.

Majaribu haya jamani, siku moja yule mama akaumwa ghafla homa kali na kutapika ikabidi mama yake atafute msaada kwa majirani wampeleke hospital wakampeleka akapimwa na kugundulika ana malaria na uti basi kurudi nyumbani na ile hali aliyokuwa naye na kuumwa tena akawa hoi mpaka mama yake akaanza kushindwa kumuuguza maana hakuweza hata kushuka kitandani.

Akawa ni mtu tu wa kulala kitandani malaria ilimdhoofisha sana, lakini MUNGU bwana sio mwanadamu akapita kijana siku moja kuulizia njia kwenye ile nyumba ndipo alipogonga na kukaribishwa ndani maana yule mama alikuwa anamlisha mwanye ndani watoto wakamwambia kwamba wapo ndani pita akamkuta yule mama anaumwa akiuguzwa na mama yake ambaye ni mzee roho ilimuuma sana na akamuomba mama awe anamuuguza yule mdada..yani mtu ulitaka kuelekezwa njia akaishia kuwa msaada mkuu huyu MUNGU jamani.

Basi kijana akawa anatoka kwao mbali na hapo anakuja kwa mwanamke kumuuguza kila siku uguza uguza na wewe lakini kwa mpango wa MUNGU yule mama akafa, yule kijana aliumia sana kama alikuwa anamjuwa tokea mwanzo basi taratibu za kumzika zikaanza kufanyika, ikabidi wamtafute baba watoto wake wampe habari yule baba akawajibu kwamba yupo njiani anaenda safari hawezi kuja wamzike tu..mmhh watu waliumia kweli mtu ni mkeo na amekuzalia watoto mmetengana ndio leo huoni umuhimu wake.

Watu na ndugu wakafanya msiba na kuuzika mwili siku ya tatu wanampigia yule baba kuhusu watoto wake anasema hawezi kuja kuwachukuwa watafutiwe sehemu wakae, basi kuna kaka mmoja ambaye alikuwa ni mjomba wa marehemu akasema basi yeye angewachukuwa mkewe akakasirika sana na kumwambia kama utawachukuwa utafute na housegirl wa kuwaangalia maana yeye hana huo muda!!!!!

Mpaka tunapewa hizi habari wale watoto walikuwa kwa bibi yao, yani roho inaniuma mimi haswa kwakuwa nilikuwa na mjuwa alikuwa mdada mzuri ana roho nzuri, inaniuma sana kwakuwa yani mtu hata kama mmeachana huoni umuhimu wa watoto wako ugomvi wako na mke wako unawahusu nini watoto wataishia mitaani wewe ukila raha,halafu sisi wanawake yani mwanamke unakuwa huna huruma na mtoto wa mwanamke mwenzio kweli unakataa kumtunza unaona mzigo wewe unajuwa kesho yakikukuta atakutunza nani mumeo?? wakati tena unaweza kuta mwanaume ukiumwa yeye ndio kapata visa ya kutoka nje na kustarehe, ni wanaume wachache sana utaumwa akuuguze kwa upendo na ukweli mpaka upone, mwanamke unakuwa huna huruma na watoto ambao hawajakukosea kitu, jamani wanawake tujifunze.

Ukishakuwa mwanamke MUNGU amekupa sense ya sita ya ziada ni kuwa na moyo wa chuma, mangapi tunafanyiwa mabaya lakini bado tupo pamoja na kulea familia zetu lakini mwanaume akitikiswa kidogo tu na mkewe na nyumba ana hama na anatafuta mahawara kumi wa kumtoa mawazo..ukishakuwa na kujijuwa wewe ni mwanamke lazima ujuwe unajukumu la kujitunza wewe na jamii nzima ni jukumu lako kusaidia pale unapoweza hata kwa mawazo tu ndio maana wanasema ukielimisha mwanamke unaelimisha jamii sasa wanawake wasikuhizi ni wabinafsi, wachoyo, wanafki jamani...tujirekebishe kwakweli fanya mema na MUNGU atakulipa usisubiri kulipwa na binadamu maana utasubiri sana.


Sunday, May 26, 2013

Nimeikuta hii sehemu...Mabig sasa tutafanyaje na siye wengine hizi ndio starehe zetu

This summary is not available. Please click here to view the post.

Thursday, May 23, 2013

Kisa kingine cha Mahouse gals....mmmhh hatareeeeeeee

Basi kuna mdada huko sitamtaja jina naamin watu waweza mtambua aliagizaga housegal mahali akaletewa sasa mume wa huyo dada si mtembezi ni wale waume ambao akitoka kazini yuko home akitoka home yuko kazini......
yule baba alikuwa mnywaji wa pombe lakin ananywea home huku anaangalia tv...mama mwenye nyumba yeye alikuwaga anachelewa kurudi kutokana na majukumu ya kikazi.....sasa bwana.....bi housegal akaanza mbwembwe mume wa mwenzake akikaa kuanza kujinywea bia na yeye anafungua friji anavuta story anakaa karibu na hubby anakunywa bia.....mume akaona mmmh huyu bi dada kulikoni tena....lakini hakumsemesha sema wanakuwa busy kama wateja walokutana bar...kila mtu na bia yake......
housegal akaona hàitoshi akaànza kuwa mara analegeza kifungo cha shati au anavaa ka gauni kepesi alafu kila bia ikiisha anamfungulia mwanaume nyingine yaani akajiari uweitres mweee mbaba vikamshinda akamwambia mkewe sitaki hii mbuzi ndan kwangu.....mké hapana mme wangu anafanya kazi vizuri na kweli alikuwa mchapa kazi haswaaaa.........


mume akagoma sasa akasemma kama hutaki naondoka mimi ndo akakubali haya mdogo wanngu ondoka.......msichana wakati anapanga nguo mama mwenyenyumba akamfata kumpa pesa na kumuaga.......binti akasema na una bahati ungechelewa kidooooogo ungeondoka wewe....heee mama sindio kashangaaa

kumbe bi dada ni mshirikina wa kutupwa kuna kadada kalikuwa kanamsikia anaongea na simu saaa babu mbona nafata maelekezo yako lakin mtu mwenyewe haelekei nimefulia dawa kwenye nguo zake nimefanya kama ulivosema babu lakin holaaaa...............kumbe mwanaume harogeki yuleeeeeee

Kumbe msichana wa kazi alikuwa anataka kumloga baba achukuliwe yeye kuwa mama mwenye nyumba na mkewe afukuzwe.

Mariam

Inasikitisha sana...part 2

asa yule binti tuliyeishia story yake jana, baada ya kufika pale na kuombewa, ndugu , yalipanda mapepo hayo, tena bora pepo, sasa hili lilikuwa ni JINI MAHABA, mpo hapo? likaelezea weeee, na mwishowe ikabidi tu kusalimu amri na kuondoka, ndo yule binti kufunguliwa na kuanza kujielezea kwamba ni kweli huwa anateswa na majini. sasa wandugu, hili jini pale nyumbani mnadhani lisingeleta madhara yoyote? uharibifu, mafarakano, n.k?


Zifuatazo ha simulizi halisi ambazo nimeziona mie mwenyewe kwa macho!

Kuna mama fulani pale mjini kati, alipata housegelo, kumbe yule binti alikuwa ni mchawi, alikuwa anajigawa mara mbili katika kufanyakzi zake, nyumba ile ni ya ghorofa, pale upanga, kwa hiyo at the same time, yuko jikoni anapika na yupo bafuni anafua, mpo hapo?
Kuna mwingine huyu ni shangazi wa staff mwenzangu, yeye alipata binti wa hivyo pia, huyu sasa alikua akienda kuwanga usiku na ungo, anaondoka na mtoto wa boss wake mdogo, anambeba mgongoni na kupaa naye, ili tu asilie huku chumbani wakati yeye akitoka, kwa hiyo anaamua kuruka, naye, afya ya huyu mtoto ilikuwa mbaya sna kwa sababu ya baridi, na mbu waliokuwa wanamuuma kila siku.

Kuna huyu mwingine hapo Kibangu kwa shosti yangu vile vile, halafu wamama haya mambo ya kutuma tu nauli uletewe binti kama unaagiza vocha dukani haipendezi! jirani yake alikuwa anaenda kwao mahenge likizo, akampa nauli kwamba amletee housegelo, without knowing kwamba huyu jirani yake "si mwema", kurudi akaja kweli na binti, kumbe walikuja na ungo, sasa kuna kosa alifanya kwenye hii familia ya shoti wangu, akachukua Ubongo wa mtoto wa shosti, kwa hiyo yule mtoto akawa taahira ghafla, yaani zezeta kabisa kwa kutoa udenda, nafupisha tu kwamba, baada ya kumuomba Mungu kwa muda mrefu, binti mwenyewe akakiri kwamba ni yeye ndo amemfanya Joshua kuwa zezeta, aliagizwa na mama wa jirani wamle nyama, wakashindwa kwa sababu wazazi "wanasali sana', wakaamua kumfanya zezeta ili kuwakomoa, sasa basi walipoamua kumrudisha kwao, ndo akasema mie siwezi kurudi na bus, kwani mlikujaje? tulikua na ungo! mpo hapo? ndo huyu shosti wangu kujua kwamba kumbe jirani yake alikuwa ni wa ulimwengu ule wa kule "chini'.

Sasa basi it happened, shosti yangu fulani akawa naye anashida sana ya msichana wa kazi maana ana mtoto mdogo, nikamshauri amwombe Mungu while anatafuta na sio akurupuke tu kutuma nauli mikoani, si nikaanza kumweleze hii stiry ya hapo juu? Without knowing kumbe kwa simulizi ile, ni Mungu alikuwa anamfungua macho ili ajue binti yake anayetaka kumwondoa yukoje! my darling friends, unaweza kuona hizi ni story tu hazikujengi wewe, kumbe ikawa ni namna fulani Mungu anaitumia kusema na mtu fulani humu ndani!

Guess what? Kesho yake anatoka kazini (alikuwa ni daktari wa Police oysterbay), kwa hiyo saa kumi anafika nyumbani, akakuta binti anapoza uji ampe mtoto wake, mhh! akasikia sauti moyoni inamwambia, hebu muulize binti ameweka nini kwenye uji wa mtoto? hakupingana na ile sauti, authoritatively, akamwuliza dada, umeweka nini kwenye uji? mhh! hapo ndipo mziki ulianza, mind you ni jana tu nilitoka kumpa story ya huyo binti wa Kibangu aliyemloga Joshua, mtoto wa shosti yangu. Hee, binti si akasema nimeweka " dawa", kuulizwa dawa gani kwani mtoto anaumwa? Mind you ni daktari huyo mama, binti akajibu, kwani mama hujui kama mimi ni mchawi? Mhh! shosti wangu akatoa macho , akaanza kuuliza vingine alivyofanya mle kwenye ile familia, wandugu binti akasema, huwa nawawekea bafuni maji ya kuoga ya maiti, unayapata wapi, akasema mama wa nyumba ya pili ana kisima chake kule uani kwake, kwa hiyo huwa ananipa niwawekee bafuni, sasa nyie wamama mnaowekewa maji ya kuoga na wasichana ndo mfunguke macho! enhee, kingine? akasema unaona hizo goroli anachezea Rayan? akasema hayo ni macho ya paka, wala sio goroli,uwiii, rafiki yangu alipiga kelele watu wakajaa,jamani sio mbali ni pale Tabata Liwiti, akasema, ukinituma kusafisha chumbani kwako nimeweka dawa chini ya godoro lenu ili" msiweze" halafu uachike,niolewe mie, uwiiiiiiii! wandugu, sio habari ya kubuni nimeona live kwa shosti wangu, kwa hiyo tunaposema spiritual screening huwa huwa ni MUHIMU SANA.
Ni pale tu uhusiano wetu na Mungu unapokuwa mzuri, ndipo tunapokuwa na AUTHORITY ya kuweza "kufanya hizo screening", maana tulipewa hayo Mamlaka in accordance with the Holy Scripture.
Wandugu,tunamuhitaji Mungu sana in every aspect of our lives, so we should be connected with Him always, huyo ni Mungu yule, aliyemzuia Balaam njiani asiende kuwalaani Israel, ni huyo huyo aliyemwonya Yusufu katika njozi,kwamba aondoke akimbilie Misri yeye na mkewe Mariam maana kesho yake Herode alipanga kuua watoto wa kiume, na huyo Mungu aweza kukuamsha wewe usiku na kukuonyesha adui anayetaka kuja kuangamiza nyumba yako, stay connected with Him always, for your safety and security.Sasa ya kumalizia, ni juzi, last saturday, nilienda kumpeleka msichana wangu kwenye maombi kanisani, maana huwa anaweweseka sana usiku. Tukafika pale, tukakuta kuna "Osigelo' anaombewa, nikamuuliza yule mama niliyekaa naye jirani, aisee huyu binti ni mwanao? akasema ni msichana wangu wa kazi, ana shida gani? akasema ni "mchawi" , umejuaje? kasema nimekaa naye wiki moja tu vitu anavyovifanya vimenipelekea kumwuliza na amekiri, vituko gani? anachelewa kurudi nyumbani asubuhi, mhh! kurudi kutoka wapi? akasema tukilala usiku huwa anatoroka, anaenda wapi? kuzimu na bibi yake? hee? Huyo bibi yake unaishi naye? hapana, huwa anamfuata usiku wanaondoka, milango yote tunafunga, lakini binti anatoweka anarudi asububi saa nne, hee? macho yalinitoka kama fundi saa! umemtoa wapi? nilimpa mtu nauli akaniletea, huko Iringa, hee? she is just 16 years old, wandugu niliona mwenyewe juzi, yule binti alieleza mambo mengi sna wakti akiombewa, na kwamba yeye mission yake ni nini anapopata kazi za ndani kwenye nyumba za watu!

Mhh! hebu leo niishie hapa, kesho tumalizie na yule wa shosti yangu wa pale Tabata mawenzi, yeye hakuwa mchawi, lakini alichokifanya, kinatisha! MY darling friends, Tunamuhitaji sna Mungu, na sio kwa wafanya kazi wa ndani tu , but hata na ndugu tunao ishi nao au wageni wanaotutembelea makwetu, hivi mnajuwa huwa wanawafanyia nini watoto wetu usiku wanapolala vyumbani kwao?


Kesho tutamalizia!

Mwenye macho haambiwi tazama!

Stella

Mabig...ndoa hizi part 2:

Basi jumatatu akaondoka baada ya ushauri akarudi kwake.jion mwanaume alivyotoka kazin km kawaida yake akaja kwa bidada kumuangalia maana alimdanganya anaumwa.
akamlazimisha hadi akampeleka hosp.kucheki malaria bidada akawa na mdudu mmoja akamchukulia dawa wakarudi kwa bidada.kwa vile mdada bado alikuwa anatafakari akawa hana furaha.mwanaume akawa anajitahd kumchangamsha changamsha akiamini mdada anaumwa
kijana hajaondoka hadi asubuhi.asubuh ilipofika akaenda kazini akarudi mchana.ili wadiscuss hyo issue maana mdada alimwambia ana maongezi nae.akamwambia ya prisca ofisi hakukalik nataka kujua una mazungumzo gani ila nakuomba twende b'myo tutafute hotel nzuri tulale hadi kesho ndo tutaenda kuongelea huko naamini kila kitu kitakua poa mdada akakubali akajiandaa wakaenda kwenye saa nane hv hapo ilikuwa jumanne.
kufika huko mwanaume kaomba hadi kalia.hataki waachane.hadi kawa km amechanganyikiwa.na bidada akamwambia ndoto zangu ilikuwa nije niwe na mume hvyo umeniharibia maisha kijana akamwambia ameshajua cha kufanya hvyo bidada awe na amani wakalala.
sasa leo jumatano wakatoka bmoyo akamrudisha mdada home yeye akaenda kwa ofisi
kama saa saba akarudi na wazo kua hataki mdada ateseke hvyo ameamua kumuacha mke wake rasmi ili abaki na bidada kwa madai alikuwa anaishi nae kwa ajili ya watoto na anaona hao wawili wamekua wakubwa atawapeleka boarding huyo wa miez tisa atamchukua akifika miaka miaka 3 wakabishabana maana mdada anaona huruma kwa mke mkubwa japo nae anampenda jamaa.
kijana kasema anamwachia mkewe kila kitu coz hataki kumuumiza.nyumba na stationery anayomiliki mkewe hatavigusa.
sasa kilichonifanya nimalizie huu umbea ni jamaa kaja jion kwenye saa nne kabeba bag kubwa km mbili eti wakae hapo kwa bidada kwa mda huku wanatafuta nyumba nzima wapange.ndo bidada haelewi maana anampenda na anaonea huruma familia yake.amechanganyikiwa maana atakua km ameolewa na kwao wanajua ana mimba ila wanajua anaishi mwenyewe.

Bado tunataka kujuwa wapenzi hawa wataendeleaje..nitawaletea tena hii story maana nimeambiwa nitatumiwa tena...

MMhhh wanaume hawa!!!! unaambiwa tumekutana kimjinimjini na siku tutaachana kimjinimjini


Wednesday, May 22, 2013

Inasikitisha sana...Part 1

 kuna rafiki zangu, walioana, baada ya miezi kadhaa wakapata mtoto, but wakati wanapanga mpango wa kuoana, hawakupima afya zao kama ilivyo siku hizi, kwa sbabu they use to be "Lovers" for so long, binti akiwa form two, kaka akiwa form five, in the same school, so they didn't see the importance of being screened. Alipojifungua huyu shosti angu, mtoto alikuwa 'mnyafu nyafu', yani hakuwa na fanya nzuri, nakumbuka alizaliwa February 28, akafa February 29, mwaka uliofatia, tukaenda kuzika mkoani,but dalili za mtoto zikaonyesha kwamba alizaliwa ameathirika, baada ya msiba rafiki zangu wakashauriwa kwenda kupima, wakaonekana 'wameathirika'. Wakajihoji sna hii imetokea wapi? mbona tumekuwa waaminifu sna tangu tuko shuleni? Ndipo yule bwana akakumbuka jinsi alivyouguza familia ya baba yake mdogo kule mkoani, alivyoshambuliwa na ukimwi, sasa kwa kuwa ni enzi zile, hawakujua kama ni UKIMWI, wakasema hapana hii familia " IMELOGWA" kwa kuwa baba ni mbunge, kwa hiyo "wamewaonea wivu". walisema hivyo kwa kuwa waliugua familia nzima kwa wakati mmoja na kufa, unaambiwaa ukienda kijini kwao kule nani hii, makaburi yamejipanga kwa kufuatana!


Huyu baba mwenye nyumba alikuwa ni mbunge, mkewe akamwambia huko Dodoma mnakaa muda mrefu sna wakati wa Bunge, hebu tafuta wenyeji huko, wakutafutie msichana wa kazi, maana wa hapa mjini, sio watulivu. haya, kweli baba akafanya vile. Akaomba wenyeji wamtafutie housegelo, akapata binti wa Kirangi, mweupe pee, yaani "mwali mbichi " ng'ari ng'ar. Kumbe yule binti ni mwathirika, akasafirishwa na mh. Mbunge mpaka kwao Mbeya, akaanza kazi za ndani pale. Sasa basi, watoto wa kiume wa yule mbunge ni wakubwa, wanasoma secondary, wengine vyuo, wakija likizo, "wanapumzika kwa dada", baba yao naye, anapumzika hapo, baba wadogo wanaokaa pale nao wanajipumzisha pale, dereva wa yule mbunge naye anapumzika na mke wa mbunge yule, unaona chain hiyo? sasa muuguzaji wa ile familia akawa ndo huyu mume wa rafiki yangu, maskini, mtoto watu hakuna cha kuvaa gloves wala nini, umetoka kijijini umekuja pale kusomeshwa, inabidi uwe mtii tu, kuwaogesha kuwanawisha n.k, ndipo alipopata huu ugonjwa.

Wale wandugu walianza kufa kwa kupishana wiki tatu, mwezi, mpaka wote wakafa! Na dereva yule naye akafa na na mkewe huko alikokuwa. Kwa hiyo vitu kama hivi wandugu tusivipuuzie, usiseme mie sina watoto, kumbe una wadogo zako pale, shemeji zao, n.k! MWenye masikio na asikie!

Sasa kesho tutaangalia na screening ya kiroho pia, hii ni kwa wale mahouse gelo wachawi. Ndugu zanguni,this wolrd is not a bed of roses, ni uwanja wa vita, tumezungukwa na mambo mengi sana ya nguvu giza. Niliombwa na wifi wa mdogo wangu kumsaidia kumpokelea house girl wake stand ya mkoa pale Ubungo na kumpeleka kwake kwakuwa alikuwa na shughuli fulani akashindwa, kufika pale nyumbani, cha kwanza alichofanya ni kumsalimia house gelo na kumwambia kwamba wao ni watu gani na imani yao ni nini, na kwamba "lazima tukuombee' kwanza ndio uingie chumbani ukaoge na kuweka virago vyako, nilimwona huyu wifi sasa analeta "unyanyapaa wa kiimani" kumbe she knew what she was doing! Yalishamkuta ya kumkuta! Can you guess what Happened while praying for that house maid?



Kesho tutaendelea.

Stella

Monday, May 20, 2013

Mwanamke na Ndoa yako..halooo ngoja na mimi leo niuze sura eboo kila siku niwauzishe wengine tu, inahusu

HAYA SASA...wapi wanawake wenye ndoa zao mchakato unaanza ni kufundwa wanawake wenye ndoa zao tu shoga ni 7/7/2013 Majestic hall Sinza kwa Remmy kwanzia 11:00am-18:00pm kwa kiingilio 30,000/= hakuna sare vaa unavyotaka ila utambue kukaa ni chini hatutaweka viti kabisa, hiyo ndio heshima ya mwanamke anayefundwa"UNYEYEKEVU" kuwa tayari tunakaribia kuanza kutoa tickets..hehe heiya uuwwiii sipati picha huku ni kwa watu wazima bibi wenye mali zao ndani hawakopi na kurudisha..haloooo kama msemo umekupita poleeee...tukutane siku hiyo na kumbuka hakuna malipo ya mlangoni na mwisho wa kulipia ni 6/7

Mabig...ndoa hizi

wanaume za watu nao wamezidi kutongoza tongoza kuliko ht single boys.nina rafiki yangu yaani yeye alitongozwa bila kujua km yule mwanaume ni mume wa mtu.
Ni mwaka wa pili sasa yuko nae,amempangia na gari kamnunulia na amemuajiri kwenye kampuni yake.kila siku anampitia bidada wanaenda wote kazin,jion wakitoka anaenda kwa bidada anakaa hadi saa sita ndo anaondoka.akisafiri wako wote,yaani asilimia 95 ya mda wa mwanaume yupo na bidada.sasa kumbe kijana ana mke na amezaa nae watoto watatu.

Na mwanaume huwa anaenda na huyo dada tanga kwa wazazi na ndugu zake mara nyingi.na hamna aliemwambia kuwa kijana kaoa.zaidi wanampokea kwa nderemo na vifijo.
 
Na mwanaume alimbembeleza bidada azae nae angalau mtoto mmoja.mwanaume ni mkristo na kumbe alifunga ndoa kanisani.sasa bidada ana mimba ya miezi mitano.na mwanaume mapenzi ni moto moto.

Sasa jana kuna mfanyakazi mmoja kwenye kampuni ambayo ni ya huyo mwanaume akamwambia bidada ukweli kuwa kijana ana mke na mwanae wa kwanza ana miaka mitano.wa mwisho miezI tisa.kumbuka dada anafanya kazi kwenye kampuni ya kijana.
bidada akaamua kumuuliza kIjana maana hakuamini, walivyotoka kazini jana wakapitia mahali kula akamuulizakijana akakubali ni kweli akamtajia na majina ya watoto akamuuliza mbona hajamwambia siku zote akamwambia kila jambo na wakati wake wakati wa kukwambia ulikuwa haujafika nilijua utaumia na mimi sipendi uumie akaomba sana msamaha kwa kumficha siku zote hizo.
Bidada akamwambia nahitaji msimamo wako akamwambia nawapenda wote mke wangu tumejenga nae nyumba ndo tiunayoishi,ndo maana na wewe nakujengea.mke wangu nimemnunulia rav 4 nyekundu wewe ya silver.mke wangu anastationary kubwa ya kutengeneza macounter ndio mana na wewe nimekwambia uchague biashara maana haya maisha kuna leo na kesho.nyie wote ni wake zangu ndo mana mda wote wa mchana niko na wewe na yule usiku.sitaki kumuacha hata mmoja bi dada akachannganyikiwa hajui afanyaje.

Anaomba ushauri

Mabig...Msaada Tutani

Nimekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu na binti mmoja ambaye siku zote huwa tunafurahia mahusiano kama kawaida na hajawahi niambia mambo ya chooni...
Kilichonichanganya ni hili tukio la jana ambalo limenifanya nivunje ukimya...
Wakati tunavunja amri ya sita baada tu ya kumaliza first round tulipumzika kama kawaida ili kujiandaana second round....

Wakati niko tayari kwa second round, mrembo wangu aliomba nimpeleke chooni..."BABY NIPELEKE CHOONI"...
Nikamwambia "afadhali umesema mapema kabla sijaanza second round maana ungenikata stimu, haya baby twende..."

Nilivyo mwambia hivyo huku nikiwa nimesimama , mwenzangu aligoma, akarudia tena, "BABY NIMEKWAMBIA NIPELEKE CHOONI"....!!

Nikamwambia :"sasa si uamke twende? ..Nilivyosema hivyo, binti alianza kuniangalia kwa jicho la hasira na baadae akavaa nguo zake akatoka kwa jazba...

Kusema kweli nilipigwa na butwaa huku nikiwa sielewi kinachoendelea.Baada ya muda kidogo alinitumia text inayosema hivi:

"Mwanaume gani wewe huelewi...!!! siamini kama ni mshamba kiasi hicho. Next time nikikwambia NIPELEKE CHOONI maana yake ubadilishe mlango"

Kumbe maana yake ilikuwa kumpeleka chooni ni kumuingilia kinyume na maumbile,kitu ambacho niliapa kutotenda maishani mwangu....

 
Naombeni ushauri au mtazamo wenu.Binti bado nampenda na tuna share vitu vingi sana...Najaribu kuachana naye lakini nashindwa na Kumpeleka chooni siwezi hata kwa dawa..!!

Thursday, May 16, 2013

Hili nawe linakukuta....

TANGAZO: Kama unajijuwa wewe mpenzi/mume/mke wako ama wewe mwenyewe ni mvivu wa mzunguko juu ya huwezi zaidi ya mzunguko moja naomba uje hapa nina dawa ya kukupa tena ya kiasili haina chemicals simanajuwa mimi nacheza na asili tu..jamani na ukishatumia kama huna aibu naomba utoe majibu yake hapa..kuna mdada nimempa jumatano leo kanipigia simu na haya ndio maneno yake"Rosemary Mizizi kumanina zako mtoto mdogo halafu mchawi, jamani ndani ya nyumba sasa hatulali ni kutombana tu mwanaume anawahi kurudi na akishapumzika anataka kutombana, nachoka lakini nasikia raha mshenzi kweli wewe mwanamke"...nikatumiwa na 20,000/- ya beer...

Kama na wewe unatatizo hili karibu nikutibie...

Whatsapp na unipigie, Viber, Tango :0717 019320 ama uniinbox facebook..

Wednesday, May 15, 2013

Katika Mzunguko Tafakari haya....

KWANZA KABISA ILI UFURAHIE KUFANYA MAPENZI NI LAZIMA UFANYE NA MTU AMBAYE UNAMFEEL, HII NDIYO SHERIA YA KWANZA KUBWA SANA, YANI MTU AMBAYE AKIKUSHIKA, AKIUONGELESHA, UKIMKUMBUKA KITU KIPITE TUMBONI KIKATE CHWAAAAAAAA..

UWE NA MUDA WA KUTOSHA KUFANYA MAPENZI NA HUYO MPENZIO WAKO, SIO MUDA WA KUIBA IBA, SIO MUDA WA KUJIFICHA JIFICHA, SIO MUDA WA KUOTEA, NI LAZIMA UWE NA MUDA HASWA MAPENZI YANAHITAJI MUDA.

NILAZIMA UWE UMETULIZA AKILI, KAMA UNA REJESHO SAA NNE ASBH ALAFU UNATAKA KUTOMBANA SAA MBILI WEWE AAA,A UNAJIDANGANYA.. KAMA UNA DENI ALAFU UMEACHA SIMU ON WEWE UNAJIDANGANYA... NI LAZIMA UTULIZE AKILI YAKO, JIFUNZE KUTULIZA AKILI YAKO MTOTO WA KIKE, WANAWAKE WENGI SANA WAMEATHIRIKA AKILI ZAO NA MAMBO YA MAISHA, MAMBO BINAFSI NA MAMBO YA HASIRA NK. HII SIO NZURI JAMANI, KUFIKA KILELENI SIO JAMBO DOGO ETI, EBO.

NI LAZIMA UJUE MWILI WAKO, JUA UKISHIKWA WAPI, UNASIKIA RAHA, JUA UKIFANYWA VIPI UNASIKIA RAHA, SIO HUJUI HATA MAENEO YA MWILI WAKO, HUJUI UKIGUSWA WAPI UNASISIMKA, LA HASHA. NI LAZIMA UWE UNAJUA MWILI WAKO VYEMA.

NI LAZIMA UJIFUNZE MWILI WAKO KUWA SPECIAL, SENSTIVE , SIO KILA MTU AKUBUSU, AKUKISS, AKUSHIKE KIUNO, AKUPIGE KOFI,, SASA HATA MPENZI AKIKUBUSU UTAJUAJE? MPENZI AKIKUPIGA KOFI UTAJUAJE? (Unaweza kufikiri ni utani lakini ni hatari sana na unajikuta umeathirka haa ushikwa na mashine hustuki maana wadada wa siku hizi kubusiwa, kushikwa kiuono ni sawa kabisa, alafu saa ya sex mpenzi wako anakushika kuino hushtuki, si umeshakuwa sugu utashtukaje, ukikisiwa huoni hata si umeshazoea kukisiwa na kila mtu nyooooo , alafu unadai kufika kileleni inakucosts utafikaje?) HIVYO NI LAZIMA MWILI WAKO UWE NA HESHIMA, HESHIMU MWILI WAKO ILI UKIWA KWENYE SHUGHULI PEVU UINJOY.

EPUKA KUWA NA WAPENZI ZAIDI YA MMOJA. UNAPOKUWA NA MPENZI ZAID YA MMOJA KWA WAKATI MMOJA UNAKUWA CONFUSED, HUYU AMEZOEA KUKATIKA, HUYU AMEZOEA KUKUSHIKA MWISHO WA SIKU UNASHINDWA KUJUA UMESIMAMIA WAPI,, UNAPOKUWA NA MPENZI HAKIKISHA ANA LAST LONG ILI UJIJUE, UFURAHIE KITOMBO,, UNLELSS KAMA UNAFANYA FOR FUNNY AMA BIASHARA ILI UPATE PESA, ILA KAMA NI KWA STAREHE UNAJIDANGANYA HAKUNA PENZI LA KUSHARE TAMU LABDA UWE KUBUHU NDIPO UTAINJOY ILA KAMA. HIVYO EPUKA WAPENZI WENGI KW WAKATI MMOJA.

HAPA NDIPO PATAMU.. AIBU. UNAPOAMUA KUFANYA MAPENZI WEKA AIBU PEMBENI. UKIWA NA AIBU AIBU NDUGU ITAKUCOST ITAKUGHARIMU.. MWENZAKO ATAFIKA ANDAKO WEWE UTABAKI HAPO UMEKAA KAMA MBILI,, UKISHAMTHIBITISHA KWAMBA NI MPENZI WAKO,, SASA WEKA AIBU KUSHOTO... AKIWA JUU, AMA UKIWA JUU MWAMBIE FANYA HIVI, WEKA HIVI, KATIKA HIVI INGIZA HIVI SHIKA HIVI,,HATA KAMA NI LIZEMBE MSHIKISHE KWA NGUVU EBO... HAHAHAHAHA... MWAMBIE JAMANI NISHIKE KIUNO, INGIZA KIDOLE NAKAZALIKA. WENGI HUWA MNAONA AIBU.. AIBU SIO JAMBO ZURI KWENYE MAPENZI HASA SAA YA KUTOMBANA,, KUWA WAZI MUELEZE,,,,

WENGI WAMEKUWA WAKIPENDA KUTUMIA KILEO, KWA KUWASAIDIA KUONDOA AIBU.. FINE KAMA UNAKUNYWA SINA NENO JUU YA HILI ITS ABOUT YOU.. . LAKINI KAMA HUNYWI SASA AIBU YAKO UIONDOE, JIFUNZE KUONDOA AIBU.. KWAMA ANAINGIZA MBOO NDAN KWA NINI UONE AIBU? USIONE AIBU,, ILA KAMA UNAKUNYWA FINE. ILA SASA NA KUNYWA YENYEWE SIO YA KONYAGI, AMA SAFARI 5, PUUU

USAFI, USAFI NAO NI CHACHU YA MAPENZI, HAKIKISHA UNAKUWA MSAFI WEWE NA MWENZA WAKO ANAKUWA MSAFI, MDOMO, MIGUU KATI KATI YA VIDOLE, MATAKO, UKE, UUME, PUA, MASKIO, MAKWAPA,NI SEHEMU NYETI, BAHATI MBAYA MKASHIKANA HAYO MAENEO ALAFU MTU AKAPITISHA MKONO HUKO ALAFU ANUSE DAH! MSHIKAJI NI NOMA,, HIVYO NI VYEMA HAYA MAENEO YAKAWA SAFI SANA, NI JAMBO LA KUZINGATIA.

ENEO LILILOTULIA, WAKATI MWINGINE HILI NALO NI JAMBO LA KUZINGATIA,, KAMA UKO NYUMBANI WAJENGEE WATOTO WAKO MAZINGIRA YA KUWA NA UTULIVU WAKATI WOWOTE, HII ITAWASAIDIA SANA, WAJULISHE KWAMBA MAMA NA BABA WAKIWA WAMETULIA HAKUNA KUSUMBULIWA, SIO MKO NDO MNAANZA MARA MTOTO ANALIA MAMAAAA, KAANGUKA SIJUI KAFANYAJE, MARA GETI LINAGONGWA, MARA TV IMEONGEZWA SAAUTI, MARA MFUNIKO UMEANGUKA, MARA SIJUI NINI,, HII NAYO HUPOTEZA UMAKINI,, NA KWA WASICHANA KAMA UNAFANYIA KWAKO HALI KAZALIKA PENDA UTULIVU , SIO UNAENDELEA NA SHUGHULI KUNA SHOGA YAKO ANAJUA KWAKO AKISHAKUBALIWA NA MLINZI KUINGIA BASI ANAKUJA MOJA KWA MOJA HADI MLANGONI ANAGONGA, PUUUUU MBAKA! AMA JIRANI ANAANZA KUITA, SHERAAAAA, SHERAAAAAA, EBO? UTAFURAHIA NINI SASA HAPO? PRIVACY KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE IWE KWAKO, KWENU, KWAKE AMA HOTELINI NIJAMBO LA KUZINGATIA.

Kwanini usienjoy mzunguko inahusu..kwa raha zako bwana




Monday, May 13, 2013

Msaada Tutani..

Hellow mambo n aje mumie hongera kwa kutuelimisha kwa kwel blog yako inatusaidia sana sana.Nnajua kwa kawaida usafi kwa mwanamke n kitu cha lazima hasa ukiwa unajitambua wajibu na thamani yako.Sasa mie napata tabu nnpokuwa najiswafi kwa kutoa nywele za kwapani na huku chini huwa nawashwa na kutokwa vipele baada ya siku chache zinapokuwa zinaota wakati wa kudoo zinachoma dushelele basi tabu tupu.Je solution yake n nn?